(1) Sema: Enyi makafiri!
Ewe Muhammad! Sema: Enyi makafiri, mlio shikilia juu ya ukafiri wenu.
(2) Siabudu mnacho kiabudu;
Mimi simuabudu mnaye muabudu nyinyi badala ya Mwenyezi Mungu.
(3) Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.
Wala nyinyi si wenye kumuabudu huyo ambaye mimi namuabudu, naye ni Mwenyezi Mungu wa pekee.
(4) Wala sitaabudu mnacho abudu.
Wala mimi si mwenye kuabudu mfano wa ibada yenu, kwani nyinyi ni washirikina.
(5) Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.
Wala nyinyi si wenye kuabudu mfano wa ibada yangu, kwani hii ni Tawhidi, ibada ya Mungu Mmoja.
(6) Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.
Nyinyi mna dini yenu mnayo itakidi, na mimi nina Dini yangu aliyo niteulia Mwenyezi Mungu niishike.