(1) Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,
Sema najikinga na Mola Mlezi wa asubuhi inapo pambazuka kutokana na usiku.
(2) Na shari ya alivyo viumba,
Na shari ya kila chenye shari katika viumbe, ambavyo hapana wa kuzuia shari yao ila Mwenye kumiliki amri yao.
(3) Na shari ya giza la usiku liingiapo,
Na shari ya usiku unapo kuwa totoro.
(4) Na shari ya wanao pulizia mafundoni,
Na shari ya anaye pita baina ya watu kwa sababu ya kuwafisidi.
(5) Na shari ya hasidi anapo husudu.
Na shari ya hasidi anaye tamani iondoke neema kwa wengine.