(1) Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?
Unamjua anaye kanusha malipo na hisabu ya Akhera?
(2) Huyo ndiye anaye msukuma yatima,
Ukitaka kumjua basi ni huyo ambaye anaye msukuma yatima kwa nguvu, na anamtumilia mabavu, na anamdhulumu,
(3) Wala hahimizi kumlisha masikini.
Na wala hahimizi kulishwa masikini.
(4) Basi, ole wao wanao swali,
Maangamio yatawashukia wanao sali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Swala zao wasinafiike nazo.
(5) Ambao wanapuuza Sala zao;
Maangamio yatawashukia wanao swali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Swala zao wasinafiike nazo.
(6) Ambao wanajionyesha,
Ambao huonyesha kwa watu vitendo vyao, ili wapate cheo katika nyoyo za hao watu, na wasifiwe.
(7) Nao huku wanazuia msaada.
Na huku wanazuia hisani zao na msaada wao kwa watu