89 - Surat Al-Fajr ()

|

(1) Ninaapa kwa alfajiri.

(2) Na kwa masiku kumi.

(3) Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja.

(4) Na kwa usiku unapopita.

(5) Je, hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

(6) Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyowafanya kina A'di?

(7) Wa Iram, wenye majumba marefu?

(8) Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

(9) Na Thamudi waliochonga majabali huko bondeni?

(10) Na Firauni mwenye vigingi?

(11) Ambao walifanya jeuri katika nchi?

(12) Wakakithirisha humo ufisadi?

(13) Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

(14) Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

(15) Ama mtu anapojaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

(16) Na ama anapomjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

(17) Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima.

(18) Wala hamhimizani kulisha masikini.

(19) Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa.

(20) Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

(21) Sivyo hivyo! Itakapovunjwa ardhi vipande vipande.

(22) Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu.

(23) Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

(24) Atasema: Laiti ningelijitangulizia kwa uhai wangu!

(25) Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

(26)

(27) Ewe nafsi iliyotua!

(28) Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umeridhiwa.

(29) Basi ingia miongoni mwa waja wangu.

(30) Na ingia katika Pepo yangu.