92 - Surat Al-Lail ()

|

(1) Ninaapa kwa usiku unapofunika!

(2) Na mchana unapodhihiri!

(3) Na kwa Aliyeumba dume na jike!

(4) Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.

(5) Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu.

(6) Na akaliwafiki lililo jema.

(7) Tutamsahilishia yawe mepesi.

(8) Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake.

(9) Na akakanusha lililo jema.

(10) Tutamsahilishia yawe mazito!

(11) Na mali yake yatamfaa nini atapokuwa anadidimia?

(12) Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.

(13) Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.

(14) Basi nakuonyeni na Moto unaowaka

(15) Hatauingia ila mwovu kabisa!

(16) Anayekadhibisha na kupa mgongo.

(17) Na mcha Mungu ataepushwa nao.

(18) Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.

(19) Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliyemfanyia hisani ndio anamlipa.

(20) Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.

(21) Naye atakuja ridhika!