(1) Ninaapa kwa mbingu na Kinachokuja usiku!
(2) Na nini kitakachokujulisha ni nini hicho Kinachokuja usiku?
(3) Ni Nyota yenye mwanga mkali.
(4) Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
(5) Hebu na ajitazame mwanadamu ameumbwa kwa kitu gani?
(6) Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa.
(7) Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
(8) Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
(9) Siku zitakapodhihirishwa siri.
(10) Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
(11) Ninaapa kwa mbingu yenye marejeo!
(12) Na kwa ardhi inayopasuka!
(13) Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
(14) Wala si mzaha.
(15) Hakika wao wanapanga mpango.
(16) Na Mimi napanga mpango.
(17) Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.