91 - Surat Ash-Shams ()

|

(1) Ninaapa kwa jua na mwangaza wake!

(2) Na kwa mwezi unapolifuatia!

(3) Na kwa mchana unapolidhihirisha!

(4) Na kwa usiku unapolifunika!

(5) Na kwa mbingu na kwa aliyeijenga!

(6) Na kwa ardhi na kwa aliyeitandaza!

(7) Na kwa nafsi na kwa aliyeitengeneza!

(8) Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake.

(9) Hakika amefanikiwa aliyeitakasa.

(10) Na hakika amehasiri aliyeiviza.

(11) Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao.

(12) Aliposimama mwovu wao mkubwa.

(13) Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipowaambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

(14) Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

(15) Wala Yeye haogopi matokeo yake.