90 - Surat Al-Balad ()

|

(1) Ninaapa kwa Mji huu!

(2) Nawe unaukaa Mji huu.

(3) Na ninaapa kwa mzazi na alichokizaa.

(4) Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

(5) Ati anadhani hapana yeyote atayemuweza?

(6) Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

(7) Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

(8) Kwani hatukumpa macho mawili?

(9) Na ulimi, na midomo miwili?

(10) Na tukambainishia zote njia mbili?

(11) Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

(12) Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

(13) Kumkomboa mtumwa.

(14) Au kumlisha siku ya njaa.

(15) Yatima aliye jamaa.

(16) Au masikini aliye vumbini.

(17) Tena awe miongoni mwa walioamini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

(18) Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

(19) Lakini waliozikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

(20) Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.