(1) Ninaapa kwa tini na zaituni!
(2) Na kwa Mlima wa Sinai!
(3) Na kwa mji huu wenye amani!
(4) Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
(5) Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
(6) Lakini wale walioamini na wakatenda mema, hao watapata ujira usiokwisha.
(7) Basi ni kipi baadaye kitakachokukukadhibishia malipo?
(8) Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?