83 - Surat Al-Mutaffifin ()

|

(1) Ole wao hao wapunjao!

(2) Ambao wanapojipimia kwa watu hudai watimiziwe.

(3) Na wao wanapowapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

(4) Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa.

(5) Katika Siku iliyo kuu.

(6) Siku watakapomsimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

(7) Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

(8) Unajua nini Sijjin?

(9) Kitabu kilichoandikwa.

(10) le wao siku hiyo kwa wanaokadhibisha!

(11) Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

(12) Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

(13) Anaposomewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

(14) Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao waliokuwa wakiyachuma.

(15) Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

(16) Kisha wataingia Motoni!

(17) Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyokuwa mkiyakadhabisha.

(18) Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika Illiyyin.

(19) Na nini kitakachokujuvya nini Iliyyin?

(20) Kitabu kilichoandikwa.

(21) Wanakishuhudia waliokaribishwa.

(22) Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

(23) Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

(24) Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

(25) Watanyweshwa kinywaji safi kilichozibwa vyema.

(26) Kizibo chake ni miski. Na katika hayo na washindanie wenye kushindana.

(27) Na mchanganyiko wake ni Tasniim.

(28) Chemchemi watakayoinywa waliokurubishwa.

(29) Kwa hakika wale waliokuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walioamini.

(30) Na wanapopita karibu yao wakikonyezana.

(31) Na wanaporudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

(32) Na wanapowaona husema: Hakika hawa ndio hasa waliopotea.

(33) Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

(34) Basi leo walioamini ndio watawacheka makafiri.

(35) Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

(36) Je, makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda?