(1) Ninaapa kwa mchana!
(2) Na kwa usiku unapotanda!
(3) Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
(4) Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko uliotangulia.
(5) Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
(6) Kwani hakukukuta yatima akakupa makazi?
(7) Na akakukuta umepotea akakuongoa?
(8) Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
(9) Basi yatima usimwonee!
(10) Na anayeomba au kuuliza usimkaripie!
(11) Na neema za Mola wako Mlezi zisimulie.