55 - Surat Ar-Rahman ()

|

(1) Arrah'man (Mwingi wa Rehema).

(2) Amefundisha Qur-ani.

(3) Amemuumba mwanadamu.

(4) Akamfundisha kubaini.

(5) Jua na mwezi huenda kwa hesabu.

(6) Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.

(7) Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani.

(8) Ili msidhulumu katika mizani.

(9) Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.

(10) Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.

(11) Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.

(12) Na nafaka zenye makapi, na rehani.

(13) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha.

(14) Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo.

(15) Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.

(16) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha

(17) Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.

(18) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(19) Anaziendesha bahari mbili zikutane.

(20) Baina yake kipo kizuizi, zisiingiliane.

(21) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(22) Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.

(23) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(24) Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyoundwa kama vilima.

(25) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(26) Kila kilichoko juu yake kitatoweka.

(27) Na utabakia uso wa Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.

(28) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(29) Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.

(30) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(31) Tutakufanyieni hesabuni enyi makundi mawili.

(32) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(33) Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa mamlaka.

(34) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(35) Mtatumiwa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.

(36) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(37) Itakapopasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.

(38) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(39) Basi Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.

(40) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(41) Watajuulikana wahalifu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.

(42) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(43) Hii ndiyo Jahannamu ambayo wahalifu walikuwa wakiikanusha.

(44) Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayochemka.

(45) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(46) Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.

(47) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(48) Bustani zenye matawi yaliyotanda.

(49) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(50) Ndani yake zimo chemichemi mbili zinazopita.

(51) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(52) Humo katika kila matunda zimo namna mbili.

(53) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(54) Wawe wameegemea matandiko yenye bitana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.

(55) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(56) Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.

(57) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(58) Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.

(59) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha.

(60) Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?

(61) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(62) Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyingine mbili.

(63) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(64) Za kijani kibivu.

(65) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(66) Na chemichemi mbili zinazofurika.

(67) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(68) Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.

(69) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(70) Humo wamo wanawake wema wazuri.

(71) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(72) Wanawake wazuri wanaotawishwa katika mahema.

(73) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(74) Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.

(75) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(76) Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.

(77) Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayoikanusha?

(78) Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.