79 - Surat An-Nazi'at ()

|

(1) Ninaapa kwa wanaokomoa kwa nguvu.

(2) Na kwa wanaotoa kwa upole.

(3) Na wanaoogelea sawasawa.

(4) Wakishindana mbio kweli kweli.

(5) Wakidabiri mambo.

(6) Siku kitakapotetemeka cha kutetemeka.

(7) Kifuate cha kufuatia.

(8) Siku hiyo nyoyo zitapigapiga.

(9) Macho yatainama chini.

(10) Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?

(11) Hata tukiwa mifupa iliyobunguliwa?

(12) Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye hasara!

(13) Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu.

(14) Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!

(15) Je! Imekufikia hadithi ya Musa?

(16) Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la Tuwaa, akamwambia:

(17) Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.

(18) Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?

(19) Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.

(20) Basi alimwonyesha Ishara kubwa.

(21) akini aliikadhibisha na akaasi.

(22) Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.

(23) Akakusanya watu akanadi.

(24) Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.

(25) Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.

(26) Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanaoogopa.

(27) Je, ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliyeijenga!

(28) Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.

(29) Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.

(30) Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.

(31) Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake.

(32) Na milima akaisimamisha imara.

(33) Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.

(34) Basi itakapofika hiyo balaa kubwa,

(35) Siku ambayo mtu atakumbuka aliyoyafanya,

(36) Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,

(37) Basi ama yule aliyezidi ujeuri,

(38) Na akakhiari maisha ya dunia,

(39) Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!

(40) Na ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,

(41) Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!

(42) Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?

(43) Una nini wewe hata uitaje?

(44) Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.

(45) Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuihofu.

(46) Ni kama kwamba wao siku watakapoiona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.