101 - Surat Al-Qari'ah ()

|

(1) Inayogonga!

(2) Nini Inayogonga?

(3) Na ni nini kitachokujulisha nini Inayogonga?

(4) Siku ambayo watu watakuwa kama nondo waliotawanywa;

(5) Na milima itakuwa kama sufi zilizochambuliwa!

(6) Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito.

(7) Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.

(8) Na yule ambaye mizani zake zitakuwa hafifu.

(9) Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!

(10) Na nini kitachokujulisha nini hiyo?

(11) Ni Moto mkali!