(1) Itakapochanika mbingu.
(2) Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza.
(3) Na ardhi itakapotanuliwa.
(4) Na kuvitoa vilivyokuwa ndani yake, ikawa tupu.
(5) Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza.
(6) Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
(7) Ama atakayepewa daftari lake kwa mkono wa kulia.
(8) Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi.
(9) Na arudi kwa ahali zake na furaha.
(10) Na ama atakayepewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake.
(11) Basi huyo ataomba kuteketea.
(12) Na ataingia Motoni.
(13) Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
(14) Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
(15) Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
(16) Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapokuchwa.
(17) Na kwa usiku na unavyovikusanya.
(18) Na kwa mwezi unapopevuka.
(19) Lazima mtapanda tabaka kwa tabaka!
(20) Basi wana nini hawaamini?
(21) Na wanaposomewa Qur-ani hawasujudu?
(22) Bali waliokufuru wanakanusha tu.
(23) Na Mwenyezi Mungu anajua wanayoyadhamiria.
(24) Basi wabashirie adhabu chungu!
(25) Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usiomalizika.