44 - Surat Ad-Dukhan ()

|

(1) Ha Mim

(2) Ninaapa kwa Kitabu kinachobainisha.

(3) Hakika Sisi tumekiteremsha katika usiku uliobarikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.

(4) Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hekima.

(5) Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.

(6) Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

(7) Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.

(8) Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.

(9)

(10) Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapoleta moshi ulio dhahiri.

(11) Utakaowafunika watu. Hii ni adhabu chungu!

(12) Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.

(13) Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.

(14) Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: 'Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.'

(15) Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!

(16) Siku tutakayoyashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.

(17)

(18) Akasema: 'Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.

(19) Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.

(20) Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.

(21) Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.'

(22) Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: 'Hakika watu hawa ni wakosefu.'

(23) Mwenyezi Mungu akasema: 'Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.

(24) Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao ni jeshi litakalozamishwa.'

(25) Mabustani mangapi na chemchemi ngapi waliziacha!

(26) Na mimea na vyeo vitukufu!

(27) Na neema walizokuwa wakijistareheshea!

(28) Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.

(29) Basi mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.

(30) Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,

(31) Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.

(32) Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.

(33) Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.

(34) Hakika hawa wanasema:

(35) 'Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.

(36) Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.'

(37) Je, ni wao bora au watu wa Tubbaa' na waliokuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.

(38) Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.

(39) Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.

(40) Hakika siku ya Uamuzi ni wakati uliowekwa kwa wao wote.

(41) Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.

(42) Isipokuwa atakayemrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu mno.

(43) Hakika Mti wa Zaqqum

(44) Ni chakula cha mwenye dhambi.

(45) Kama shaba iliyoyeyushwa, hutokota matumboni.

(46) Kama kutokota kwa maji ya moto.

(47) (Itasemwa): 'Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!

(48) Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayochemka.'

(49) Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!

(50) Hakika haya ndiyo mliyokuwa mkiyatilia shaka.

(51) Hakika wacha Mungu watakuwa katika mahali pa amani.

(52) Katika mabustani na chemchemi.

(53) Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana.

(54) Hivi ndivyo itakavyokuwa, na tutawaoza mahurilaini.

(55) Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.

(56) Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu.

(57) Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

(58) Basi tumeifanya nyepesi hii Qur-ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.

(59) Ngoja tu, na wao wangoje pia.