96 - Surat Al-Alaq ()

|

(1) Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliyeumba.

(2) Amemuumba binaadamu kwa tone la damu.

(3) Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

(4) Ambaye amefundisha kwa kalamu.

(5) Kamfundisha mtu aliyokuwa hayajui.

(6) Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri.

(7) Akijiona katajirika.

(8) Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

(9) Umemuona yule anayemkataza.

(10) Mja anaposali?

(11) Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

(12) Au anaamrisha ucha Mungu?

(13) Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

(14) Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

(15) Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

(16) Shungi la uwongo, lenye makosa!

(17) Basi na awaite wenzake!

(18) Nasi tutawaita Mazabania!

(19) Hasha! Usimtii! Nawe sujudu na ujongee!